Nakushukuru Baba

Nakushukuru Baba
Performed bySt. Joseph Migori
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerAlfred Ossonga
Views7,406

Nakushukuru Baba Lyrics

  1. Nakushukuru Baba (shukuru), Baba Mwenyezi Mungu
    Mwenyezi kwa kuwa umeniumba
    Nakushukuru Baba (shukuru), Baba Mwenyezi Mungu
    Mwenyezi kwa kuwa umeniumba

    Nitakulipa nini ee Mungu, wangu cha kukupendeza wewe
    Baba mimi sina kitu chochote
    Cha kulinganisha na ukarimu wako
    Maombi yangu uyapokee, na dua zangu zikufikie
    Kwa huruma yako Baba nisamehe
    Mimi kwa makosa niliyoyatenda
    Tafadhali Baba uniongezee siku nyingi ili nikutumikie

  2. Nakutukuza Baba (tukuza), wewe ni ngome yangu
    Ngome yangu ndiwe unayenilinda
    Pokea sifa Baba (pokea) sifa ni zako wewe,
    zako wewe Baba Mwenyezi Mungu
  3. Nakuabudu Baba (abudu), Baba Mlinzi wangu -
    Mlinzi kwa kuwa wewe ni mwema
    Uniongoze Baba (ongoze), katika kweli yako,
    Kweli yako nifanye mapenzi yako
  4. Bwana nifanye mimi (nifanye), chombo cha kazi yako
    kazi yako nikutumikie wewe
    Pasipo na amani (pasipo), pasipo na upendo,
    upendo nitangaze Jina lako
  5. Usiniache Baba (ee Baba), uwe nami daima
    Daima katika maisha yangu,
    Nikufuate wewe (fuate), daima siku zote,
    siku zote milele hata milele