Ramani ya Mbinguni

Ramani ya Mbinguni
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumRamani ya Mbinguni
CategoryTafakari
ComposerC. A. L. Ndomelo
Views8,114

Ramani ya Mbinguni Lyrics

  1. Naisafisha njia (mimi) - njia iendayo Mbinguni *2
    Nilikoahidiwa (mimi) - makao ya milele mimi
    Naisafisha njia - njia iendayo Mbinguni
    Tena - Sina wasiwasi, wala - hofu ndani ya moyo
    Kwa kuwa - ninayo ramani, ramani ya mbinguni
    Tena - ninapoisoma, hii ramani ya mbinguni
    Nakiri - nitauona, upendo wa Mungu kwangu

  2. Asante Bwana Mungu - (aee) aee (aee) aee (aee)
    Kwa kunipenda mimi - ae ee aeee aee
    Ukanipa ramani - (aee) aee (aee) aee (aee)
    Ramani iniongoze inifikishe uliko ee Mungu wangu.
  3. Asante Bwana Yesu -
    Kwa kunipenda mimi -
    Ukaja duniani -
    Ili tu unikomboe unitoe utumwani mwake shetani
  4. Asante Roho mtakatifu -
    Kwa kunipenda mimi -
    Kwani huniongoza
    Katika hii safari kuelekea mbinguni kwa Mungu Baba