Rafiki Yangu Njoo

Rafiki Yangu Njoo
Performed bySt. Cecilia Isibania
CategoryTafakari
ComposerJ. Bahati
Views6,097

Rafiki Yangu Njoo Lyrics

  1. Rafiki yangu njoo kaa chini, nisikilize kwa makini
    Rafiki njoo kaa chini ,nikueleze jambo moja aah

    {Kila mtu atalipwa sawasawa na matendo ooh
    Kila mtu atalipwa sawa nayo matendo yake } * 2
  2. Kama uliua kwa upanga, utakufa kwa upanga
    Uliua kwa silaha, utakufa kwa silaha aah
  3. Kama ulikuwa ni mzinzi, utakufa kwa uzinzi
    Ulikuwa mzinifu, utakufa kwa uzinzi iih
  4. Kama ulikuwa mfitini, utalipwa ufitini
    Ulikuwa mfitini, utalipwa ufitini iih
  5. Kama ulikuwa mkarimu, utalipwa ukarimu
    Ulikuwa ni mchoyo, utalipwa sawa na choyo ooh
  6. Kama ulinitendea wema, utalipwa matendo mema
    Ulinitendea baya, utalipwa kwa ubaya aah