Furaha Hiyo Niliyo Nayo

Furaha Hiyo Niliyo Nayo
Performed bySt. Michael Otiende Lang'ata
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerM. Z. Yohana
Views3,862

Furaha Hiyo Niliyo Nayo Lyrics


  1. Furaha hiyo niliyo nayo yatoka kwa Mungu *2
    {Ndiye Baba (baba), ninayemtumaini (baba)
    Kwenye maisha yangu, Yeye ndiye kimbilio} *2 Baba

  2. Sina budi kumshangilia Mungu
    Baba kwa huruma yake na wema wake
    Mema mengi aliyonitend`a mimi
    Sina budi kushukuru asante Baba
  3. Yeye ndiye tumaini langu mimi
    Ndiye msaada wangu na wokovu wangu
    Bila Mungu mimi siwezi chochote
    Sina ujanja wowote ni ubatili
  4. Ni wangapi, walimpuuza Mungu
    Kwa kukiuka sheria wakapata fimbo
    Wakarudi, wakamlilia Mungu,
    Kuomba huruma yake, akawasamehe
  5. Nawe ndugu kujiona we mdhambi
    Mungu anakutafuta urudi kwake
    Nenda hima ukatubu dhambi zako,
    Ukaipate furaha iliyo ya kweli