Bwana Ametukuka Sana

Bwana Ametukuka Sana
Alt TitleNitamwimbia Bwana
Performed by-
CategoryTBA
ComposerRenatus Rwelamira
Views3,562

Bwana Ametukuka Sana Lyrics

BWANA AMETUKUKA SANA

  1. Ndipo Musa na (wana) wa Israeli
    wakamwimbia Bwana wakinena

    Nitamwimbia Bwana kwa kinywa changu
    Kwa maana ametukuka sana
    Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini
    Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu
    Naye amekuwa wokovu wangu
    Yeye ni Mungu wangu na baba yangu nami nitamsifu
  2. Bwana ni mtu wa vita, mtu wa vita
    Bwana ndilo jina lake jina lake
    Magari na jeshi lake Farao amewatupa baharini
    Maakida yake wateule wamezama bahari ya shamu
    Vilindi vimewafunikiza walizama vilindini kama jiwe
  3. Bwana mkono wako wa kuume
    Umepata fahari ya uwezo
    Bwana mkono wako wa kuume wawatesatesa adui
    Kwa wingi wa ukuu wawangusha chini wanaokuondokea
  4. Utawaingiza Bwana na kuwapanda
    Katika mlima wa urithi wako
    Mahali pale ulipojifanyia Bwana ili upakae
    Pale patakatifu ulipopaweka imara Bwana
    Bwana kwa mikono yako
    Bwana atatawala milele yote

    Ndipo Musa…..