Hapa We Msafiri

Hapa We Msafiri
Performed by-
CategoryMazishi
ComposerFr. G. F. Kayeta
Views9,671

Hapa We Msafiri Lyrics

  1. Hapa we msafiri simama na tazama (simama na tazama)
    Nimekufa leo, kesho - ni zamu yako
    (ona) ona vema nilivyowekwa humu,
    Na nilivyoacha mali na jamaa
  2. Nilitoka uchi tumboni mwa mamangu . . .
    Narudia uchi, kati-ka tumbo la nchi
    (Sanda) sanda moja hilo ni vazi langu,
    Wameninyang'anya hata senti moja.
  3. Nifunike vema na hilo jembe lako . . .
    Nalitangatanga, kati-ka ulimwengu
    (Basi) basi leo kiburi kimekwisha,
    Kumbe dunia hii ni mti mkavu.
  4. Nyumba yangu leo ni shimo udongoni . . .
    Hakuna mlango, haku-na madirisha
    (Kita) kitanda changu na blanketi langu,
    Ni udongo mzito wanielemea
  5. Kifafanuacho wafu mbele ya Mungu . . .
    Si cheo kikubwa, si da-raja si sifa
    (Mate-) matendo mema saa ya kufa kwangu,
    Yatafungua mlango wa uwingu
  6. Ole wangu mimi nilifanya ujinga . . .
    Kwa kuambatana, na wa-tu wa dunia
    (Ona) ona wote leo wameniacha,
    Hasa watu wale niliowapenda.
  7. Unapojiona jiwazie mwenyewe . . .
    Kufa siku moja, kwa wo-te ni lazima
    (Japo) japo sultani japo ni mtumwa,
    Mungu atamwita ikiwa saa yake.
  8. Nimekufa leo nilipona salama . . .
    Nalijidhania, mwenye - afya mwilini
    (na ma-) na mara moja nikaanguka chini
    Labda huamini kwamba nali`mzima.
  9. Yesu msalabani kateswa vikali mno . . .
    Kwa kutukomboa, aka-mwaga damuye
    Wahurumie wote wa toharani,
    Mwanga wa milele uwaangazie.
  10. Kwaherini wote kwaherini wapenzi . . .
    Ninakwenda kwetu sita-rudi nyuma
    (Kwa he-) Kwaheri Baba kwaheri Mama yangu,
    Mungu akipenda kwake tukutane.