Simba wa Israeli
Simba wa Israeli |
---|
Performed by | - |
Album | Bwana Kafufuka |
Category | TBA |
Composer | Bernard Mukasa |
Views | 3,302 |
Simba wa Israeli Lyrics
{ Simba wa Israeli anaunguruma,
Mbingu za shangwe zinatikisika, zinarukaruka
Ulimwengu wa burudani unatetemeka
Miamba mikubwa mikubwa inasambaratika } *2
{
/s/
Ni shangwe na vigelegele, nderemo chereko vifijo, kwa makofi
Shangilieni, Bwana yesu amefufuka
Manowari ya ukombozi imetia nanga
/a/
Ni shangwe na vigelegele, ni nderemo na vifijo makofi ya shangwe
Kwa furaha Mwana wa Mungu amefufuka
Manowari ya ukombozi imetia nanga
/t/
Ni shangwe, vigelegele, nderemo na vifijo
Waumini pigeni makofi, Mfalme Yesu amefufuka
Manowari ya ukombozi imetia nanga
/b/
Ni shangwe na vigelegele, nderemo chereko vifijo
shangwe shangwe, ukombozi Kristu Yesu amefufuka
ya ukombozi manowari imetia nanga
} *2
- [a] Aliyekufa mtini bila kosa,
/a/ (akakubali) kuungama na dhambi zetu, amefufuka tumetakasika milele
/s/ akakubali kuyatubu makosa yetu, ameshinda tumetakasika milele
- Hatima ya nguvu zote za shetani, (imetangazwa)
umeangusha utawala wa mwovu na tumwimbie (wote) aleluya
- Utakatifu wa mwanzo, tulioupoteza kwa dhambi
Hii Leo, ameurudisha
hesabu ya watoto wa Mungu upya tumerudishiwa
- Aliye sadaka ya agano jipya
Amedhihirisha utukufu wake machoni petu
Astahili kutukuzwa kwa sauti kuu