Amini Kuna Chakula

Amini Kuna Chakula
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Views9,163

Amini Kuna Chakula Lyrics

  1. Amin, amin, nawaambieni kuna chakula kinachowafaa,
    Nacho chakula ndicho kile cha uzima wa milele

  2. Amin kweli, nawaambieni mwanitafuta.
    Si kwa sababu mlikula ule mkate.
    Si kwa sababu mliziona zile Ishara.
    Bali sababu mlikula mkashiba *2
  3. Msikitendee kazi chakula kinachopita.
    Bali, chakula kidumucho milele.
    Chakula Musa alichowapa hakiwafai,
    Kweli Babangu anawapa kifaacho
  4. Kile chakula chenye uzima kweli ni mimi
    Ajaye kwangu hataona njaa kamwe.
    Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu
    Hukaa kwangu nami hukaa ndani yake.
  5. Hicho chakula chenye uzima kweli ni mimi.
    Kilichoshuka toka mbinguni kwa Baba.
    Mtu akila chakula hiki hatafariki.
    Bali anao ule uzima wa milele.
  6. Kile chakula ninachotoa ni mwili wangu,
    Kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.
    Msipokula huu mwili wake mwana Adamu.
    Hamna 'zima ndani yenu.
  7. Anayekula huu mwili wangu na kuinywa damu
    Ana uzima, nami nitamfufua.
    Na mwili wangu ndicho chakula kile cha kweli.
    Na damu yangu ndicho kinywaji cha kweli
  8. Na kama Baba aliye hai 'livyonituma,
    Nami ni hai, ndimi hai kwa Babangu.
    Na kadhalika, mwenye kunila ana uhai,
    Kweli nasema atakuwa hai kwangu,