Heri Hao Walio Kamili
Heri Hao Walio Kamili | |
---|---|
Choir | - |
Category | Zaburi |
Reference | Zaburi 119 |
Heri Hao Walio Kamili Lyrics
Heri hao walio kamili,
Wafuatao sheria za Bwana, na kutenda yaliyo ya haki
Heri wenye kumtii Jehova,
Na kwa moyo watamtafuta, na kufuata hizo njia zake
Naam hawakutenda ubatili, wamezifuata hizo njia zake.
Wewe umetupa mawaidha yako, ili sisi tuyatii yote.
Ningependa, njia zangu ziwe thabiti.
Ningependa, Mungu nifuate amri zako,
Ndipo mimi sitaaibika, nikifuata maagizo yako.
Ntakusifu kwa moyo wa unyofu Bwana.
Nikiisha jifunza hukumu niitatii.
Nitatii amri, usiniache *2
Jinsi gani mimi nisafishe njia yangu?
Ni kwa kutii na kufuata njia yako.
Moyo wangu umekutafuta Bwana.
Usiniache nipote mbali.
Niyaache maagizo yako moyoni.
Moyo wangu waweka neno lako,
Ee Bwana, kutenda dhambi sitaki.
Neno la Bwana litasimama imara huko mbinguni moyoni.
Moyo wangu naweka neno lako,
Ee Bwana Ee Bwana, ninakupa moyo wangu
Uniokoe niwe wako milele.
Nisife na dhambi.
Ee Bwana ninakupa moyo wangu, unipokee
Favorite Catholic Skiza Tunes
SMS the Skiza ID to 811 to get the song as your Skiza tune.
Title | SKIZA ID |
Cha Kutumaini Sina | 5814855 |
Roho Yangu na Ikuimbie | 5814859 |
Nikupe Nini Mungu Wangu | 7482438 |
Sasa Wakati Umefika | 7482439 |
Nitakwenda Mimi Mwenyewe | 7482440 |
Zaeni Matunda Mema | 5814860 |
Bwana Kama Wewe Ungehesabu Maovu Yetu | 7482444 |
Huniongoza Mwokozi | 5814856 |
Utukuzwe Ewe Baba | 7482441 |
Tazama Tazama | 7482442 |