Heri Yenu

Heri Yenu
Performed by-
CategoryHarusi
Views5,189

Heri Yenu Lyrics

  1. Heri yenu Mungu amewaunganisha,
    Msitengane mkavunje hili agano.

  2. Aliumba wazazi wetu kale, paradizoni waitawale.
  3. Alimwumba Adamu babu yetu, na Eva mzazi wetu wa kwanza.
  4. Akasema, 'zaeni mkaenee, ijazeni dunia na watu.'
  5. Leo Mungu amewabarikia, mkafunge agano tukufu.
  6. Lishikeni agano takatifu, siku zote za maisha yenu.
  7. Pete yenu kwa kweli, ni muungano waivaayo wasiachane.
  8. Enendeni wawili tangu leo, miongoni mwa raha na taabu.
  9. Nyumba yenu ijae upendano, akosaye atubu mapema.
  10. Na amani ya wenye kumcha Mungu, iwavutie nyoyo za watu.
  11. Sioni, pendo, subira na heshima, ziwe msingi wa maisha yenu.