Upendo na Ukarimu

Upendo na Ukarimu
Performed by-
CategoryLove
ComposerBernard Mukasa
Views4,482

Upendo na Ukarimu Lyrics

  1. Watu wengi tunajaribu upendo
    Tunawajali wale wanaotuhusu
    Tunaojua wataweza kutulipa
    Hatuwathamini wale wasiotuhusu
    Wala wasiojiweza, lakini

    {Leo tumejifunza wote,
    upendo ni kitu gani (wapendwa)
    Tena tumepewa mfano,
    ukarimu una sifa gani (wapenzi) } * 2

  2. Tunawakopesha wenye kipato kikubwa
    Tukiamini nao watatukopesha
    Wakitujia wenye shida na fukara
    Tunawakimbia eti hawakopesheki
    Na wana madeni mengi, lakini
  3. Wakiugua wenye nafasi za juu
    Tunajazana kwao na vichupachupa
    Tukiamini na sisi tukiugua
    Watalundikana kwetu na vifuko fuko
    Kadi na michango mingi, lakini
  4. Tukitembelewa na mtu mwenye viraka
    Tunauliza kama tulimualika
    Akija aliyeshuka kwenye shangingi
    Tunamwuliza kinywaji anachokunywa
    Tena kwa unyenyekevu lakini