Mbona Mmegeuka

Mbona Mmegeuka
Alt TitleMlipokea Nguvu ya Mungu
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views3,455

Mbona Mmegeuka Lyrics

  1. Mlipokea nguvu ya Mungu ya kushinda tamaa
    Siku ile mlipobatizwa,
    Mkaahidi kumkataa, Ibilisi na vyake,
    Sasa vipi muwe wabinafsi
    Hamshibishwi kwa riziki yenu,
    Aliyowapimia Mungu wenu
    Mnatafuna riziki ya hao walio wadogo
    Mnakula rushwa ndugu zangu

  2. Uhai na nguvu mlivyojaliwa, si kwa ajili yenu,
    Ni kwa ajili ya wahitaji
  3. Elimu mliyoipata wapendwa, si utukufu wenu
    Akatukuzwe Muumba wenu
  4. Fedha navyo vyeo mlivyoazimwa
    Jembe la Mungu wenu, mkatumikie shamba lake
  5. Acheni umimi acheni ulafi, ingawa kuna leo
    Kumbuka kwamba na kesho ipo
  6. Kipimo mnachowawia wadogo, hicho kitatumika
    Usoni penu siku ya mwisho