Mbona Mmegeuka
Mbona Mmegeuka |
---|
Alt Title | Mlipokea Nguvu ya Mungu |
Performed by | - |
Category | Tafakari |
Composer | Bernard Mukasa |
Views | 3,455 |
Mbona Mmegeuka Lyrics
Mlipokea nguvu ya Mungu ya kushinda tamaa
Siku ile mlipobatizwa,
Mkaahidi kumkataa, Ibilisi na vyake,
Sasa vipi muwe wabinafsi
Hamshibishwi kwa riziki yenu,
Aliyowapimia Mungu wenu
Mnatafuna riziki ya hao walio wadogo
Mnakula rushwa ndugu zangu
- Uhai na nguvu mlivyojaliwa, si kwa ajili yenu,
Ni kwa ajili ya wahitaji
- Elimu mliyoipata wapendwa, si utukufu wenu
Akatukuzwe Muumba wenu
- Fedha navyo vyeo mlivyoazimwa
Jembe la Mungu wenu, mkatumikie shamba lake
- Acheni umimi acheni ulafi, ingawa kuna leo
Kumbuka kwamba na kesho ipo
- Kipimo mnachowawia wadogo, hicho kitatumika
Usoni penu siku ya mwisho