Mchaka Mchaka Twendeni Mbio Mbio

Mchaka Mchaka Twendeni Mbio Mbio
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerVictor Aloyce Murishiwa
Views7,152

Mchaka Mchaka Twendeni Mbio Mbio Lyrics

  1. La mgambo sasa limelia tembea ndugu yangu tena ukaze mwendo
    Safari yetu bado ni ndefu tushikane tutembee pamoja
    Milima pia nayo mabonde, tazama visije kuwa ni vikwazo kwako
    Ubebapo Neno lake Mungu songa mbele usirudi nyuma

    {Hima hima twendeni kwa pamoja
    Mchaka mchaka twendeni mbio mbio
    aee iye ye he he he hehe
    aee iye ye he he he iye
    Twendeni wote mbinguni kwa Baba} *2

  2. Watu wengi wana mali nyingi lakini kutoa sadaka kwao ni ndoto
    Wengi wao bila kuogopa humpa Mungu wao chenji
    Wengine huwatesa wajane jamani tena kuwanyanyapaa yatima
    Ikiwa unaitamani mbingu tenda wema na twende pamoja
  3. Tuzingatie tabia yako nao wale wenzetu pia tuwasaidie
    Badala ya kusubiri wafe na kutazama kwenye misiba
    Kumbukeni maneno ya Yesu aliyonena kupitia Injili Luka
    Mimi nilipokuwa mgonjwa hamkuja kunitazama
  4. Wengine wamekataa toba husema siwezi kutubu kwa mwanadamu
    Wamesahau ya kwamba Mungu alituachia makasisi
    Amewapatia mamlaka hakika watakalolifunga duniani
    Na mbinguni pia itafungwa ole wenu mnaowadharau