Nitumwe Mimi

Nitumwe Mimi
Alt TitleKidole Juu
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views4,357

Nitumwe Mimi Lyrics

  1. // utangulizi //

    Hayo mliyofunuliwa, bila kuyalipia kitu, (nayo) ndiyo,
    Yale mliyotumwa, kwenda kwa walio wadogo
    Mungu alowatunukia awe mkuu pekee yake
    (Jiulize) nani kwenu (aliyeomba) kuzaliwa!
    (Jiulize tena) nani kwenu (anaijua) siku ya kufa!
    Hakuna! Hakuna! ha!

    // kiitikio //

    Hakuna jambo mnalomiliki hapa duniani
    Yote mliyo nayo yana mwenyewe mnamjua
    Naye amewapa haya kusudi mtumikiane
    Ili kusiwepo na matabaka miongoni mwenu
    Hiyo ndiyo hekima - ee aa ee
    [b:] Hiyo ni hekima ni hekima tele
    Hiyo ndiyo hekima -ee aa ee
    Ndugu hiyo ndiyo hekima ya kweli


    // mashairi //
  2. Kama mliyo nayo yote yangekuwa yenu
    Hiyo pumzi mnayojivunia wapendwa,
    Isingekuwa inakiogopa kichomi
    Ingeendele-a hata palipo kichomi!
  3. Uzuri wa sura zenu zenye ngozi laini
    Inakuwaje hamuwezi kuelekeza,
    Usiungue hata kwenye maji ya moto
    Na usioze unapolala kaburini!
  4. Elimu na vyeo vyenu na mamlaka yenu
    Akili nyingi ufundi navyo vipaji vyenu,
    Mbona hamvitumii mkiwa usingizini
    Na mnaota ndoto sawa na za watoto!

    // hitimisho //

    Basi mimi, ninahimizwa, kujiepusha, kujiinua
    Nijishushe mbele ya wote, wawe wakubwa au wadogo
    Nisijiinue kati ya watu hata siku moja,
    Badala yake nijinyenyekeze ili nifikike,
    Akihitajika atakayewatumikia watu
    Nijitokeze kwa haraka ili wanitume mimi, daima

    Nijitokeze kusudi wanitume mimi
    Nijitokeze, kuitikia wito daima
    Nijitokeze kusudi wanitume mimi
    Na nikitumwa niwe mwaminifu daima
    Nijitokeze kusudi wanitume mimi
    Nijitokeze wanitume na Mungu atukuzwe daima
    Nijitokeze kusudi wanitume mimi

    Nijitokeze, nijitokeze leo
    Nijitokeze kusudi wanitume mimi
    Nijitokeze, nijitokeze daima
    Nijitokeze kusudi wanitumie mimi, milele!