Tu Mavumbi Sisi

Tu Mavumbi Sisi
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Views10,534

Tu Mavumbi Sisi Lyrics

  • { Siku zinapita, miaka yapita
    Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2
  • Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2
  • mmmm mmmm mmm siku hiyo ni ya huzuni mno
    mmmm mmmm mmm siku hiyo kweli inatisha
  • Kwa maana siku hiyo,
    Mavazi yako yatakuwa ni sanda
    Kitanda chako kitakuwa jeneza
    Na nyumba yako iyakuwa kaburi
    Jamaa zako watakutupia udongo,
    kwa heri ya milele!
  • Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2
  • { Roho ndiyo roho ndiyo itiayo uzima
    Mwili haufai kitu } * 2
  • Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini
  • Tazameni mimea, shambani
    Matunda na maua, vyapendeza
    Vyote vitanyauka
    Wanyama wa pori, na nyumbani
    Na ndege angani, wapendeza
    Wote wataangamia
  • Ee ndugu sasa utubu rudi
    Mrudie Mungu wako
    Kwa maana duniani sisi ni wasafiri
    Hujui saa na siku ndugu ya kuiacha dunia
    Kwa maana duniani sisi ni wasafiri
  • Sayari angani zapendeza
    Mito na mabonde duniani
    Vyote vitatokomea
    Mungu ndiye peke ajuaye
    Siri ya maisha ya viumbe
    Vyake ulimwenguni
  • { Siku zinapita, miaka yapita
    Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2
    Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini * 2