Bwana Yesu Twakumbuka

Bwana Yesu Twakumbuka
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumHii ni Kwaresma
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Views3,916

Bwana Yesu Twakumbuka Lyrics

BWANA YESU TWAKUMBUKA

  1. Bwana Yesu twakumbuka
    Mateso yako makuu
    Ili utuokoe sisi
    Bustanini Getsemani
    Uchungu ukakupata
    Ukikumbuka dhambi zetu

    Taji la miiba wavikwa
    Na mijeredi wapigwa
    Ni mateso gani hayo
    Jasho la damu latona
    Mwili mzima ni mateso
    Yote yo kwa ajili yetu
  2. Kwa Pilato unafika
    Bure unashtakiwa
    Umekosa nini wewe Yesu
    Sisi twasitahili hukumu
    Sio wewe Bwana Yesu
    Ndiyo sisi siyo wewe

    Msalaba ni mzito
    Umeshinda nguvu zako
    Hata chini waanguka
    Askari wakupiga
    Tena bila ya huruma
    We uliye muumba wao
  3. Njiani unaonana
    Na mamayo Maria
    Mwilio wajaa madonda
    Kwa uchungu Mama MAria
    Alipomwona mwanaye
    Machozi yalimtoka

    Huku na huku wakuvuta
    Wauwaji hawa wabaya
    Kwa nguvu wakutupa chini
    Ee Yesu tusaidie
    Tujue kutubu hima
    Tuangukapo madhambini