Pendo la Marafiki

Pendo la Marafiki
Alt TitleNinyi Ndinyi Mmenikamilisha
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumAsifiwe Bwana Mungu (Vol 8)
CategoryLove
ComposerMartin M. Munywoki
Views2,836

Pendo la Marafiki Lyrics

  1. // u t a n g u l i z i //

    Ninyi ndinyi mmenikamilisha kamilisha (hadi)
    Hadi nikawa hi-vi mi-mi nilivyo (ndugu zangu)
    Ni Mungu Baba ndiye aliyetukutanisha (japo)
    Japo hatulingani tumekamilishana
    {Katika pendo lenu - ndipo nimeelewa jinsi Mungu alivyo
    Nimemuona - Mungu macho kwa macho } *2

    // k i i t i k i o //

    [ s ] Nikiwa na njaa -
    Ni ninyi marafiki zangu mnimegeao mkate
    [ a ] Penye machungu na maumivu makali -
    Ni ninyi marafiki zangu mwaniuguza majeraha
    [ t ] Nikitawaliwa na hofu -
    Ni ninyi marafiki zangu mnaonipa moyo upya
    [ b ] Tena nikipotea njia -
    Ni ninyi marafiki zangu mwanirudi mwanikosoa


    // m a s h a i r i //
  2. Ona tunavyosaidiana hima, wenyewe kwa wenyewe,
    Wakati wa furaha hata wa shida
    Tumeweka mbali tofauti kidaraja na mali
    Bahati iliyoje kuwa pamoja
  3. Ona chuki, wivu, fitina, umimi, havimo kati yetu
    Wakati wa furaha hata wa shida
    Tumeweka msingi imara usiotikisika
    Bahati iliyoje kuwa pamoja

    // h i t i m i s h o //
    { Pendo pendo pendo pendo -
    pendo letu lidumu milele
    Tuombeane tusaidianeni -
    waone Mungu kati yetu } *2
    Wasitenganishwe - wapendanao
    Waombeeni - baraka tele
    sitenganishwe - wapendanao
    Waombeeni - baraka tele, pendo na lidumu