Mungu ni Upendo

Mungu ni Upendo
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMimina Neema
CategoryLove
ComposerE. F. Jissu
Views14,836

Mungu ni Upendo Lyrics

  1. Mungu ni upendo, tupendane *4 ae ae

    Tufuateni upendo na kutaka karama za rohoni *2
    Lakini zaidi mpate mpate kutubu *2 ae ae

    { Nijaposema kwa lugha za wanadamu na malaika
    Mimi kama mimi sina upendo - nimekuwa shaba iliayo (mimi)
    Nijaposema kwa ndimi za wanadamu na malaika
    Mimi kama mimi sina upendo - nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao } *2

  2. Tena nijapokuwa na unabii,
    Na kujua siri zote na maarifa yote
    Nijapokuwa na imani kamilifu
    Kiasi cha kuweza kuhamisha milima
    Kama sina upendo, si kitu mimi!

    Tena nikitoa mali zangu zote, kuwalisha maskini
    Tena nikijitoa mwili wangu, niungue moto
    Kama sina upendo, si kitu mimi!
  3. Upendo huvumilia, hufadhili
    Upendo hauhusudu, hautakabari
    Upendo haujivuni, haujivuni

    Haukosi kuwa na adabu
    Hautafuti mambo yake
    Hauoni uchungu
    Hauhesabu mabaya
    Haufurahi udhalimu
    Bali hufurahi pamoja na ukweli
    Huvumilia yote
    Huamini yote
    Hutumaini yote
    Hustahimili yote

    Upendo upendo upendo ni kila kitu