Lo Ajabu Kupata Uzima

Lo Ajabu Kupata Uzima
Alt TitleAnd Can It Be
Performed bySauti Tamu Melodies
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerCharles Wesley
VideoWatch on YouTube
Views6,277

Lo Ajabu Kupata Uzima Lyrics

  1. Lo! Ajabu kupata uzima,
    Katika damu ya Mwokozi wangu
    Aliyenifia pendoni
    Mimi niliyemsulubisha
    Upendo huu wa kushangaza kabisa
    Wewe Yesu wangu kunifia pendoni

    { Upe - upendo huu,
    Nashaa- nashangaa,
    Yesu - Yesu wangu kunifilia } * 2
  2. Yesu wangu alitoa damu
    Siwezi kuelewa neno hili
    Viumbe vyote vya Mbinguni
    Navyo haviwezi kufahamu
    Najua tu ni kwa rehema zake Mungu
    Malaika watu wote wamsujudu mno

    { Ni re - ni rehema
    Tumwa - tumwabudu
    Tumwa - tumwamini ndiye Mwokozi } * 2
  3. Aliondoka kule mbinguni
    Kwa nyumba yake Mungu Baba yake
    Na utukufu aliacha
    Afe kwa ajili ya maovu
    Rehema zake ni nyingi na ukarimu
    Kwani Mungu wangu aliniokoa mimi

    { Sista - sistahili
    Neema - neema zake
    Laki - lakini alinioka } * 2
  4. Roho yangu ilifungwa sana
    Dhambi na giza vilinilemea
    Akaniangaza rohoni
    Gereza langu likang'aa mno
    Ikafunguka minyororo yangu yote
    Nikaondoka nikaanza kumfuata

    { Siku - siku ile
    Nika - nikapata
    Uhu - uhuru kweli kwake Mungu } * 2
  5. Hukumuni mimi simo sasa
    Mimi ni wake Yesu ndiye wangu
    Yeye ni kichwa changu kweli
    Na amenivika haki yake
    Mimi hodari sasa kwa kiti cha enzi
    Napewa taji ya milele katika Yesu

    { Sina - sina hofu
    Kuso - kusogea
    Kati - katika Bwana wangu Kristo } * 2