Acheni Kukata Tamaa
| Acheni Kukata Tamaa | |
|---|---|
| Performed by | St. Cecilia Mirerani | 
| Album | Maajabu ya Mungu | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Views | 22,970 | 
Acheni Kukata Tamaa Lyrics
- {Mwenyezi ameniumba, akanileta kati yenu,
 Niwakumbushe watu wake thamani yenu duniani} *2
 {Acheni acheni kufa moyo,
 Acheni acheni kukata tama
 Yeye aliyewaumba anaijua kazi yake } *2
- Aliijua siri yenu hata kabla hamjaumbwa,
 Ramani ya maisha yenu, yote imo mikononi mwake
 Magonjwa yanayowatesa na maumivu yasiyokoma,
 Ni madogo kuliko yale aliyoyaponya kwa sekunde
- Hali mbaya ya kiuchumi, mlo mmoja madeni mengi
 Ni njia ya kunyenyekea na kumpa Mungu ukuu
 Misiba inayowaliza mnapofiwa na ndugu zenu,
 Ni njia ya wapendwa wenu kwenda mbinguni wakafurahi
- Maumivu ya kuonewa kudhulumiwa kusingiziwa
 Ni nafasi ya kusamehe na kujivika utakatifu
 Matatizo ya ndoa zenu na migogoro ya familia,
 Ni bahati mmejaliwa ya kujifunza uvumilivu
- Bebeni misalaba yenu, nyamazeni msinung'unike
 Huo ndio wokovu wenu shikilieni msiachie
 
  
         
                            