Acheni Mimi
| Acheni Mimi | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mshike Mshike (Vol 5) | 
| Category | Entrance / Mwanzo | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 10,004 | 
Acheni Mimi Lyrics
- { Acheni mimi, nimuimbie Muumba wangu,
 Aliyeniumba, mimi kiumbe mwenye akili } *2
 Aliyenipa uwezo wa kusimama hapa
 Tangu tumboni mwa mama amenipa uhai
 Juzi jana leo nimeamka kesho ajua yeye
 Maisha yangu ayapa maziwa ni kama mtoto
 { Acheni mimi, nizitamke sifa za Mungu wangu
 Na sitachoka, kumuimbia mimi ningali hai } *2
- [ b ] Nalala jioni na kuamka pia nazo nguvu,
 Ninafanya kazi na kujipatia riziki zangu
- Amenipatia akili yangu na wangu ubunifu,
 Shuleni kazini ninayoyafanya hayana pungufu,
- Mara nyingi sana ninajiuliza nitampa nini,
 Kwani Bwana amenitendea mengi bila ya kwa nini
- Ninapokuwa nazo shida nyingi hunipa tulizo,
 Kwake kila mara watu wote hupata burudiko.
 
  
         
                            