Alhamisi Kuu

Alhamisi Kuu
Performed by-
CategoryAlhamisi Kuu
Composer(traditional)
Views11,465

Alhamisi Kuu Lyrics

  1. Alhamisi kuu Yesu alituwekea
    Ekaristia takatifu, chakula cha roho

    Tuimbe - tuimbe,
    Tumshukuru - tumshukuru Yesu, mkombozi wetu
    Tuimbe - tuimbe,
    Tumshukuru - tumshukuru Yesu, sadaka yetu

  2. Yesu alishika mkate akaubariki
    Akawapa wafuasi, ndio mwili wangu
  3. Na kikombe cha divai akakibariki
    Akasema, nyweni nyote, ndiyo damu yangu
  4. Yesu aliwapa amri wanafunzi wake
    Fanyeni hivi daima kwa kunikumbuka
  5. Kisha Yesu akaenda apate kuteswa
    Akafuta dhambi zetu msalabani juu
  6. Yesu anatutolea mwili na damuye
    Naye Baba wa mbinguni anatubariki
Wimbo huu unaweza kuimbwa Siku ya Alhamisi Kuu au wakati wa Komunyo