Amkeni Tufanye Shangwe

Amkeni Tufanye Shangwe
Performed bySt. Anthoney Malindi
AlbumMalindi Kuna Nini
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerAlfred Ossonga
Views10,902

Amkeni Tufanye Shangwe Lyrics

  1. Amkeni wapenzi tufanye shangwe
    (Kweli) hekaluni mwa Mungu wetu
    Amkeni wapenzi tufanye shangwe
    (Kweli) hekaluni mwa Mungu wetu
    {Kwa vigelegele, na kwa makofi,
    Kwa machezo pia kwa nderemo
    Tumsifu Yahweh Jehova leo asubuhi *2}

  2. Waumini wote wenye moyo safi njooni tuingie kwa Bwana
    Njooni tuabudu njooni tusujudu pia tupigeni makofi
    Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
    Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie
  3. Enyi Baba njooni tusali pamoja ndani ya nyumba yake Baba
    Enyi mama njoni pigeni kelele mbele za Bwana Mungu wetu
    Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
    Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie
  4. Ameumba mbingu ameumba nchi ameumba viumbe vyote,
    Bahari ni yake mito na milima ahimidiwe Mungu wetu
    Njooni tuimbeimbe tuchezecheze turukaruke leo
    Njooni hekaluni mwa Bwana tufurahi na tushangilie