Asante Bwana kwa ukarimu

Asante Bwana kwa ukarimu
Performed by-
CategoryThanksgiving / Shukrani
Views5,551

Asante Bwana kwa ukarimu Lyrics

  1. Asante Bwana kwa ukarimu wako wa ajabu,
    Na fadhili zako hazina mipaka,
    Sina budi kusema Bwana asante

    Umenijua Bwana kabla sijazaliwa
    Maisha yangu umeweka kwenye msitari
    Kwa maana umenipenda, umenijali
    Nakushukuru ee Bwana asante *2

  2. Ninapotafakari upendo wako kwangu mimi
    Na riziki zangu wanipa kila siku
    Nashindwa nikulipe nini ee Bwana
  3. Na mwili wangu umenipa akili ya kutosha
    Kuliko wanyama utashi umenipa
    Ufananishwe na nani ee Bwana
  4. Uhai wangu umenipa na sasa niko hai
    Wengi wamezikwa mimi bado nahema
    Nikulipe nini kwa upendo wako
  5. Na marafiki ndugu jamaa Bwana umenipa
    Dhiki zikinizidi wanifariji
    Upendo wako Bwana unanishangaza.
  6. Kwa hayo yote siwezi lipa langu shukrani
    na mengi bado hata siwezi kusema
    Bwana unayotenda kwangu makuu