Asilegee Moyowe
| Asilegee Moyowe | |
|---|---|
|  | |
| Alt Title | Asiregee Moyowe | 
| Performed by | St. Joseph Cathedral Dar-es-Salaam | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | (traditional) | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 31,725 | 
Asilegee Moyowe Lyrics
- Asilegee moyowe, asitokwe machozi,
 Akimkumbuka Munguwe, kwa yake makombozi,
 Mtoa roho msalabani, mtaka kufa mwenyewe,
 Kwa sababu kumpenda ni, nani mfunga moyowe?
- Bustani mle Getsemani, amwomba Mungu Baba,
 Je mtu Mungu ana nini?, nguvu zake ni haba,
 Rabbi wangu waziona, dhambi za binadamu,
 Mwili wako umetona, kama jasho la damu.
- "Salamu Rabi salamu", anena Yuda mbaya,
 Mwenye moyo wake mgumu, ambusu pasi haya,
 Aliwaambia “basi, ntakayembusu ndiye,
 Mtwaeni na kwa upesi”, Yuda nani nisiye.
- Yuda nani ila yeye, aliyetenda dhambi?
 Akikosa kwa Munguwe, mtenda kwa hia na mbi,
 Mwenye kumtendea mema, mtaka dhambi haoni,
 Kwamba ni kutupa neema, kumwendea shetani.
- Wote ni kupiga mbio, mitumewe pamoja,
 Wamtia mikono yao, askari walokuja,
 Wampeleka hukumuni, aamuliwe na mtu,
 Ye kutoka uwinguni, Mwanzi mkuu wa watu.
- Mtume Petri amkanusha, amenena “simjui”,
 Uhodari umekwisha, machoye hainui,
 Pilato amwona Rabbi, hakukosa 'ta neno,
 Asema “sioni dhambi”, lakini ni mwoga mno.
- Athubutu kumwachia, “si hukumu” aomba,
 “Mmoja nitamfungulia, Yesu au Baraba,
 Wayahudi mwamtakani?", “Baraba aachwe tu,
 Yesu afe msalabani, damuye juu yetu”
- Pilato “hukumu gani? simo nanawa mkono,
 Mkimtaka Yesu mwueni”, la mwamzi hilo neno,
 Mara askari wamwanza, ni kupiga kelele,
 Kumcheka na kumchokoza, mwenye mema milele.
Asiregee Moyowe is a traditional piece.
The piece has been harmonized and arranged by various composers, the most common piece being John Mgandu's harmony (1986) based on a French traditional melody, “Jésus-Christ monte qu Calvaire”.
The song has been recorded by several choirs among them St. Patrick Morogoro, St. Augustine Mavurunza Dsm
  
 
 
 
  
         
                            