Bwana Nakupenda

Bwana Nakupenda
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumNakaza Mwendo (Vol 19-20)
CategoryZaburi
Views7,629

Bwana Nakupenda Lyrics

  1. Bwana nakupenda we Mungu wangu
    Pembe ya wokovu na nguvu yangu
    Wewe ndiwe mwamba na jabali langu
    Nakimbilia kwako Mwokozi wangu
    Bwana ndiye kinga na ngao yangu
    Yeye ndiye mwamba na ngome yangu
    Bwana ndiye kinga na ngao yangu
    Sitaogopa nimwogope nani
    {Kwa hiyo nitamwita astahili sifa
    aniokoe na adui zangu *2

  2. [t/b] Asifiwe Mungu aliye hai atukuzwe Mungu wokovu wangu
    [s/a] Asifiwe mwamba wa usalama, atukuzwe kati ya mataifa
    [t/b] Ampa mfalme wokovu wote, wokovu mkuu ampatia
    [s/a] Amfanyia fadhili masihi humjalia mteule wake
    [t/a] Kwa hiyo nitaliimbia sifa jina lako Mungu wangu
  3. Kamba za kifo zilinizingira, maangamizi yalinivamia
    Kamba za kuzimu zilinisonga, mitego ya kifo ilinikabili
    Katika tabu nilimwita Mungu nilimlilia anisaidie
    Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake alisikia
    Kilio changu kilimfikia masikioni mwake
  4. Hapo ndipo dunia ikatetemeka ilihangaika na kutikisika
    Misingi ya milima ikayumbayumba Mungu alikuwa amekasirika
    Moshi ulishuka puani mwake moto uvunjao kinywani mwake
    Aliinamisha anga akashuka chini na wingu jeusi miguuni pake
    Makaa mengi ya moto yakalipuka kutoka kwake
  5. Mungu alinguruma kutoka mbinguni mkuu akatoa sauti yake
    Alipulika giza mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka
    Huko mawinguni makaa ya moto mvua ya mawe zikatokea
    Alirusha umeme ukawapiga maadui zake wakatawanyika
    Hapo ndipo bahari na dunia zilipoonekana
  6. Mungu alinyoosha mkono wake kutoka juu akanichukua
    Katika maji mengi alininyanyua akanitoa kwa adui zangu
    Tegemeo langu ni Bwana Mungu aliniokoa na adui zangu
    Walioniwinda aliwatisha aliwakemea wakapotea
    Amenitoa hapo akanipeleka palipo na nafasi