Ee Bwana Uisikie Haki
| Ee Bwana Uisikie Haki | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) |
| Album | Tazameni Miujiza (Vol 2) |
| Category | Zaburi |
| Composer | J. C. Shomaly |
| Views | 3,911 |
Ee Bwana Uisikie Haki Lyrics
Ee Bwana uisikie haki, usikie haki
Utege sikio lako Bwana, kwa maombi yangu (Bwana)
{ Usikilize maombi yangu yasiyotoka katika,
Yasiyotoka katika midomo ya hila } *2- Nyayo zangu zimeshikamana, zimeshikamana na njia zako,
Hatua zangu haziku, hazikuondoshwa. - Ee Mungu nimekuita wewe, kwa maana wewe utaitika,
Utege sikio lako nisikie mimi. - Unifiche chini ya uvuli, chini ya uvuli wa mbawa zako
Niamkapo nishibishwe kwa sura yako.