Bwana Unayoyatenda
| Bwana Unayoyatenda | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mbinguni Kutakuwa Raha (Vol 4) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 5,503 | 
Bwana Unayoyatenda Lyrics
- { Bwana unayoyatenda kwangu mimi ni huruma ya kweli
 (ya kweli) sitakuwa na fadhila nisipokiri haya } *2
 { Kuniumba, bila ya kukwambia, akili yangu tofauti sana
 Ninalala pia ninaamka tazama niko hai } *2
- Uhai nilio nao, sijanunua lolote,
 Bwana nashukuru sana ninasema asante
- Marafiki umenipa, maisha ya kupendeza,
 Bwana nashukuru sana ninasema asante
- Umenipa na watoto, yote sikutarajia,
 Bwana nashukuru sana ninasema asante
- Yote umetenda kwangu, bila mimi kuwa mwema
 Bwana nashukuru sana ninasema asante
 
  
         
                            