Bwana yu Mwema

Bwana yu Mwema
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumIkulu ya Mbinguni
CategoryTBA
Views4,098

Bwana yu Mwema Lyrics

  1. Njooni wenzangu, tuimbe pamoja
    Njooni tumwimbie Bwana, kwa kuwa Bwana yu mwema *2
    Amenitendea mambo mema mengi
    Mambo mengi ya ajabu kweli Bwana yu mwema *2

    Haya njooni, njooni tumwimbie Bwana
    Tuimbe kwa shangwe, kwa shangwe na nderemo nyingi
    Vigelegele, tumpigie vigelegele hoyee hoye
  2. Njooni tumshangilie, kwa shangwe na nderemo
    tumpigie makofi, na vigelegele vingi
    kwa furaha tuimbe, filimbi tuvipige
    Tujifunge na vibwebwe, tumshangilie Bwana
  3. Nilikata tamaa kwamba nimeshashibndwa
    Bwana akanipa moyo, nami nikafanikiwa
    Akanipa uwezo, wa kuyashinda yote
    Nikashinda kwa kishindo, kweli Bwana yu mwema
  4. Bwana hakuniacha, watesi wafurahi
    Akawapiga kikumbo, kwa nguvu wakaanguka
    Nikamililia, Bwana Mungu wangu,
    Baba Baba wasamehe, hawajui watendalo
  5. Nguvu zaanza kwisha, sauti yakauka
    Wenzangu endeleeni kumsifu Mungu Baba
    Siyo kwamba natoka, au nimeshachoka
    Bali ninavuta nguvu, nije kumwimbia Bwana