Chozi la Damu

Chozi la Damu
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMungu Yule
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views22,828

Chozi la Damu Lyrics

  1. Watoto wa nyumba zote njooni tuungane
    Tuwalilie wazazi chozi la damu
    Tupaaze sauti zetu za majonzi na kwikwi
    Kwa wachache wenye huruma watatusikia
    Haki ya malezi bora tumenyang'anywa
    Urithi wa maadili tumefutiwa
    Oh dunia dunia, dunia unatutesa
    Oh dunia dunia, tumekukosea nini
    Oh dunia dunia, mbona hupendi watoto
    Oh dunia dunia, sikia kilio chetu

  2. Oh dada zetu na mama zetu, tunajua mnajipenda
    Ingawaje tungetamani na sisi mtufikirie
    Mavazi mnayovaa leo yanatufundisha nini
    Mnafikiria nini kwa kizazi mnachokilea
    Msije mkashangaa dunia siku zinazokuja
    Viwanda vyote vya nguo vitakapofungwa
  3. Oh kila siku tunapolala baba zetu hamjarudi
    Asubuhi tukiamka, baba zetu mmeondoka
    Siku tukibahatika kushtuka usiku wa giza
    Tunachokishuhudia ni mama anapigwa makofi
    Na vitisho vya talaka matusi na harufu ya pombe
    Darasa gani mnatupa watoto wenu
  4. Oh tukirudi toka shuleni, madaftari hamkagui
    Eti kwa kuwa tumechoka, burudani mwatuwekea
    Video mnazowasha picha za vita na mauaji
    Au mikanda iliyorekodiwa Sodom na Gomora
    Hamkumbuki ya kuwa mnayafuta ya darasani
    Urithi gani mnatupa wazazi wetu
  5. Oh kwenye chakula cha usiku, siku zote baba hayuko,
    Kusali sala za pamoja, kwenye nyumba yetu ni mwiko,
    Amechelewa kutoka kwa mama mdogo yule wa siri
    Au giza likizidi, hatarudi mpaka asubuhi
    Na mama akishajua mbio kwa Anko wa usiseme`
    Familia moja baba na mama watano
  6. Oh kwa sababu ya mambo haya, ndugu zetu wanaumia
    Wapo wanaorandaranda mitaani bila makazi
    Wengi wamelazimika kuajiriwa bado wadogo
    Hawana tena nafasi ya kusoma wapate elimu
    Na wengi wanajiuza miili yao ili waishi
    Mbona dunia umetugeuka watoto