Tembea Nami Bwana
| Tembea Nami Bwana | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | Kidole Juu (Vol 23) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | C. A. L. Ndomelo | 
| Views | 10,238 | 
Tembea Nami Bwana Lyrics
- {Ee Bwana Mungu wangu
 Tembea nami usiniache kwenye dunia (hiyo)
 Ya machafuko } *2
 Nikianguka, Bwana, uniinue Bwana
 Nikiteleza, Bwana, unishike mkono
 Uniepushe na maadui wa roho yangu
 Uniepushe na maadui wa roho yangu
- Tazama ninaishi kwa mashaka na hofu kubwa
 (Kwani) Baadhi ya wanadamu wenzangu wamegeuka
 Kuwa ni maadui zangu,
 Wananiwinda wanikamate wavinyokoe viungo,
 Eti wajipatie mali.
- Tazama ninaishi kwa mashaka na hofu kubwa
 (Kwani) Baadhi yawaathirika wenzangu wamekamatwa
 Bwana na wameshauawa,
 Wamewakata vichwa na mikono, na miguu yao Bwana,
 Eti wajipatie mali
- Tazama sisi wanao wakiwa twakimbilia (kwako)
 (Kwako) twazikabidhi roho zetu mikononi mwako
 Maana ni wewe kimbilio
 Usituachie adui zako watutie mikononi
 Bwana utushike mkono
 
  
         
                            