Hebu Jiulize
   
    
     
         
          
            Hebu Jiulize Lyrics
 
             
            
- {Hebu jiulize lingetolewa tangazo leo
 Ya kwamba kila apumuaye
 na ailipie pumzi avutayo } *2
 Ni nani angejificha asilipe kodi,
 Ni nani angesema yeye ni masikini,
 Ni nani angekwepa kwani yeye ni tajiri
 Ni nani angekuwa kweli mtu wa kiburi
 Ni nani angekwepa kweli kulipia kodi (nasema)
 Ni nani angependa kunyang'anywa uhai wake * 2
- Tazama sasa majirani zako wote,
 Hakuna unayeongea naye
 Kwani unawadharau
 kwa kuwa wao hawana fedha kama zako
 Hebu tazama baadhi ya ndugu zako,
 Hupendi hata kuwaona kwako
 Unawakana kwa kuwa, wao ni maskini,
 tena unawaona ni wachafu.
- Kwa nini hivyo, biashara zako,
 wewe unawaajiri wafanya kazi
 Tena ni wachapa kazi na mwisho wa mwezi,
 huwafichia eti wameiba
 Hebu tazama wapoteza fedha nyingi,
 unapokuwa baa na marafiki
 Kwa ajili tu ya anasa, na kuwasaidia,
 maskini kwako ni hasara
- Jitafakari, fungua na legeza moyo wako
 kwa kuwajali wasiojiweza
 Na wenye shida mbalimbali, na sio kuegeza
 Hazina ya moyowe kwa shetani.