Hii Ndiyo Siku
| Hii Ndiyo Siku | |
|---|---|
| Performed by | Our Lady of Fatima Kongowea | 
| Album | Kila Mwenye Pumzi (vol 4) | 
| Category | Entrance / Mwanzo | 
| Views | 10,069 | 
Hii Ndiyo Siku Lyrics
- Hii ndiyo siku, aloifanya Bwana *2
 Tuishangilie, na kuifurahiya *2
 {Tupige makofi na vigelegele
 Sote turuke juu tumshukuru Mungu } *2
- Ndiwe Mungu wangu nami nitakushukuru
 Ndiwe Mungu wangu nami nitakutukuza
 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
 Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
- Nifungulieni malango ya haki,
 Nitaingia mimi na kumshukuru Mungu
 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
 Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
- Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa
 Mkono wa Bwana hutenda makuu
 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
 Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
- Mshukuruni Bwana kwa kuwa yeye ni mwema
 Kwa maana fadhili zake ni za milele
 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote
 Kwa mema yote Bwana uliyonijalia
 
  
         
                            