Hii ni Karamu

Hii ni Karamu
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Composer(traditional)
Views11,441

Hii ni Karamu Lyrics

  1. Hii ni karamu, uzima wa roho,
    Yumo Bwana Yesu, kwa mwili wake, kweli na damu yake

  2. Alisema Bwana twaeni wote, mle ni mwili wangu
  3. Alisema Bwana twaeni wote, mnywe ni damu yangu
  4. Nasi twasadiki ni mwili wake, kweli na damu yake
  5. Alituamuru kufanya hivyo, kwa ukumbusho wake
  6. Tukifanya hivyo tunatangaza, kifo cha Bwana Yesu
  7. Kwa hii karamu, Twashiriki uzima wa Bwana wetu
  8. Huu ni upendo aliotuachia, mkombozi wetu
  9. Hapa duniani twaishi na Baba, kwa karamu hii
  10. Na huko mbinguni tutaishi, na Baba milele yote