Huyu Ni Yule Yesu

Huyu Ni Yule Yesu
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumUzuri wa Yesu
CategoryJumapili ya Matawi (Palm Sunday)
ComposerAlfred Ossonga
Views15,073

Huyu Ni Yule Yesu Lyrics

  1. Huyu ni yule Yesu, Yesu mwana wa Daudi
    Huyu ni yule Yesu, Mwana wa Galilaya

  2. Mwambieni Binti Sayuni, tazama mfalme wako
    Anakuja kwako mpole amepanda mwanapunda*2
  3. Inukeni enyi malango, inueni vichwa vyenu
    Mfalme apate ingia, mfalme wa utukufu *2
  4. Na watoto wa Wayahudi, Walimlaki Mwokozi
    Wakiyachukua matawi, wakipiga makelele *2
  5. Aliyakemea mawimbi, Bahari ikatulia
    Akatembea juu ya maji, akatembea kwa miguu*2
  6. Aliponya wagonjwa wengi kwa neno la kinywa chake
    Hata vazi lake ni dawa, yule mama alipona *2
  7. Alimfufua Lazaro, Lazaro aliyekufa
    Akarudi tena mzima akatoka kaburi *2
Recorded by * St. Joseph Migori (Uzuri wa Yesu album) * St. Kizito Makuburi Dsm (Nyumba ya Roho album)