Isemavyo Torati
| Isemavyo Torati | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mshike Mshike (Vol 5) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 4,117 | 
Isemavyo Torati Lyrics
- { Isemavyo torati ya kale, jicho kwa jicho, jino kwa jino
 Mkuki kwa mkuki, hiyo silaha ya mababu } *2
 { Lakini mimi, ninawaambia, nawaambia,
 Msilipize kisasi kwa mambo haya } *2
 Akupigaye shavu lako moja, mgeuzie na la pili
 Akunyang'anyaye na joho lako -
 Mpe pia kanzu yako, utayashinda majaribu.
- Ndugu nawaambia nyinyi, jifunzeni kusameheana
 Acheni chuki ubinafsi, hazisaidii kwa vyovyote.
 Ukikosewa samehe, sababu hata wewe wakosea
 Mungu asingesamehe, wewe na mimi tungekuwa wapi
- Wewe unayemchukia huyu, huyu ameumbwa naye Mungu
 Kumbuka wote sisi twapita, hakuna aishiye milele
 Wamuua huyu na wewe, utakufa siku moja kama yeye
 Utajibu nini kwa Mungu, kuifanya kazi yake bila ruhusa
- Riziki aitoa Mungu, acha wivu pia masengenyo
 Mwenzako amepata kwa jasho, fanya bidii ufanikiwe
 Wamwonea wivu kwa nini, na kuanza kuharibu na kuiba
 Utajibu nini kwa Mungu, kuharibu nchi yake aliyoumba
 
  
         
                            