Kama Kunguru
| Kama Kunguru | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Habari Tuliyoleta (Vol 6) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 5,013 | 
Kama Kunguru Lyrics
- { Kama kunguru arukapo juu ya jalala kubwa
 Akitafuta mizoga na wadudu
 Alishibishe tumbo lake } *2
 { Ndivyo moyo wake mtu asiyempenda Mungu
 Utakuwa wa kubabaika na kuhangaika
 Hatakuwa na amani,
 Atakuwa kama kunguru tu, kama kunguru tu,
 Awindaye toka macheo ya jua hata yapata mawio
 Na tumbo lake bado ni tupu } *2
- Moyo wako ndugu mbona waubabaisha,
 Kutwa kucha wewe umemsahau Mungu
 Dunia ina mambo yake - tena yanapita
- Kama una kiu na tamaa za dunia
 Zina mwisho wake kwanza mtafute Mungu
 Mungu alishapanga yako - hivyo umuombe
 
  
         
                            