Kidole Juu

Kidole Juu
Alt TitleNitumwe Mimi
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumKidole Juu (Vol 23)
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerBernard Mukasa
Views25,506

Kidole Juu Lyrics

  1. //utangulizi//

    Hayo mliyofunuliwa, bila kuyalipia kitu,
    Nayo ndiyo yale mliyotumwa,
    Kwenda kwa walio wadogo
    Mungu alowatunukia awe mkuu peke yake
    (Jiulize) nani kwenu (aliyeomba) kuzaliwa!
    (Jiulize tena) nani kwenu (anayejua) siku ya kufa!
    Hakuna! Hakuna! ha!

    Hakuna jambo mnalomiliki hapa duniani
    Yote mliyo nayo yana mwenyewe mnamjua
    Naye amewapa haya kusudi mtumikiane
    Ili kusiwepo na matabaka miongoni mwenu
    Hiyo ndiyo hekima - eeh aah eeh
    Hiyo ndiyo hekima - eeh aah eeh
    Ndugu hiyo ndiyo hekima ya kweli } *2

  2. Kama mliyo nayo yote yangekuwa yenu
    Hiyo pumzi mnayojivunia wapendwa,
    Isingekuwa inakiogopa kichomi
    Ingeendele-a hata palipo kichomi!
  3. Uzuri wa sura zenu zenye ngozi laini
    Inakuwaje hamuwezi kuuelekeza,
    Usiungue hata kwenye maji ya moto
    Na usioze unapolala kaburini!
  4. Elimu na vyeo vyenu na mamlaka yenu
    Akili nyingi ufundi navyo vipaji vyenu,
    Mbona hamvitumii nyi mkiwa usingizini
    Na mnaota ndoto sawa na za watoto!

    //hitimisho//

    Basi mimi, ninahimizwa, kujiepusha, kujiinua
    Nijishushe, mbele ya wote,
    Wawe wakubwa, au wadogo
    Nisijiinue kati ya watu hata siku moja,
    Badala yake nijinyenyekeze ili nifikike,

    Akihitajika atakayewatumikia watu
    Niinue kidole juu kusudi wanitume mimi, daima
    Kidole juu kusudi wanitume mimi
    Kidole juu, kuitikia wito daima
    Kidole juu, kusudi wanitume mimi
    Na nikitumwa niwe mwaminifu daima
    Kidole juu, kusudi wanitume mimi
    Kidole juu wanitume na Mungu atukuzwe daima
    Kidole juu, kusudi wanitume mimi

    Kidole juu, kidole juu, leo
    Kidole juu, kusudi wanitume mimi
    Kidole juu, kidole juu, daima
    Kidole juu, kusudi wanitumie mimi, milele!
Second version of this song is Nitumwe Mimi, that replaces the words 'Kidole Juu kusudi wanitume mimi' with 'nijitokeze kusudi wanitume mimi' And alters the title to 'Nitumwe Mimi'