Kila Kunapokucha
   
    
     
        | Kila Kunapokucha | 
|---|
| Performed by | - | 
| Category | Tafakari | 
| Views | 4,469 | 
Kila Kunapokucha Lyrics
 
             
            
- { Kila kunapokucha, ndugu zangu mimi
 Wananikwepa na kunikimbia
 Majirani zangu wanatazamana bila kunitamkia neno
 Ewe Muumba wangu najiuliza na kujitafakari mimi
 Au nimekuwa na sura ya simba,
 Au nimekuwa na sura ya chui, hata ninatisha } *2
- Ninapokaa chini na kutafakari mwenendo wangu
 Kwani uko vipi mimi niliupenda,
 Japo magumu mimi niliyapata,
 Nilivaa sura ya kifalme pasipo kuwa na utu
- Nikiupekua pekua moyo wangu unanitisha
 Ni huo tena kwa kudhamiria
 Kwa kauli toka kwa ulimi wangu
 Nilifanana na jitu baya tena limezalo watu
- Hakuna adui hakuna rafiki kwangu wote sawa
 Hakuna mwema katika moyo wangu
 Wala rafiki katika roho yangu
 Nilijifananisha na chui tena chui mwenye njaa