Kimya ni Cha Nini

Kimya ni Cha Nini
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Views3,100

Kimya ni Cha Nini Lyrics

  1. Kimya kimya ni cha nini Bwana Yesu ametualika
    Kushiriki karamu yake, karamu ya mapendo
    Siku ile iliyotangulia kifo chake
    (Aliwaita wanafunzi wake) *2 akawaambia

  2. Huu ndio mwili wangu utakaotolewa kwa ajili yenu
    Kuleni huu ili mpate uzima wa milele,
    (Haya basi amkeni (‘mke-ni) ‘mkeni basi amkeni
    kushiriki uzima mtukufu kwa karamu ya Bwana }*2
  3. Hii ndiyo damu yangu itakayotolewa kwa ajili yenu
    Kunyweni hii ili mpate uzima wa milele
    (Haya basi amkeni (‘mke-ni) ‘mkeni basi amkeni
    kushiriki uzima mtukufu kwa karamu ya Bwana }*2
  4. Amini ninawaambieni alaye mwili na kunywa damu
    Bila kustahili atahukumiwa siku ya mwisho,
    Lakini alaye mwili na kunywa damu kwa kustahili
    Nitamfufua siku ya mwisho
    (Haya basi amkeni (‘mke-ni) ‘mkeni basi amkeni
    kushiriki uzima mtukufu kwa karamu ya Bwana }*2