Kisha Nikaona
Kisha Nikaona | |
---|---|
Choir | St. Joseph Migori |
Album | Mabawa |
Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) |
Composer | Alfred Ossonga |
Kisha Nikaona Lyrics
Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya
Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya
{ Nikauona mji (mji ule), ule mtakatifu
Jerusalem mpya ukishuka toka mbinguni } *2
-
Kwa maana mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza,
Zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena -
Nikasikia sauti kubwa ikitoka,
Kwenye kiti cha enzi, tazama maskani yake Mungu -
Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao,
Naye atayafuta, machozi katika macho yao -
Mauti maombolezo kilio maumivu,
Hayatakuwapo, tazama yote yamekuwa mapya