Kwa Nyimbo Nzuri
Kwa Nyimbo Nzuri Lyrics
- Kwa nyimbo nzuri za furaha,
njooni nyote mbele za Bwana
Kwa shangwe na vigelegele,
tumwimbie Mfalme wetu
Mataifa yote simameni mbele zake Bwana,
Makabila yote njoni leo nazo ngoma zenu
Chezeni mbele za Bwana!
{ Wajaluo na waimbe nyimbo
Wamasai na waruke juu
Wabaluhyia na wapige ngoma
Wakikuyu na wacheze sana,
Watu wote sisimukeni,
Shangwe nderemo na kelele, pigeni makofi } *2
- Vinanda vifijo kelele,
makofi machezo nderemo
Kusifu kweli kwawapasa,
enyi wanyofu wa moyo
- Pigieni Mungu kelele,
imbeni utukufu wake
Tukuzeni sifa za Mungu,
tangazeni matendo yake
- Shukuruni Bwana kwa zeze,
kwa kinanda cha nyuzi kumi
Mfanyieni Bwana shangwe,
mtumikieni kwa furaha