Kwa Nyimbo Nzuri

Kwa Nyimbo Nzuri
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNitachezacheza
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerAlfred Ossonga
Views11,345

Kwa Nyimbo Nzuri Lyrics

  1. Kwa nyimbo nzuri za furaha,
    njooni nyote mbele za Bwana
    Kwa shangwe na vigelegele,
    tumwimbie Mfalme wetu

    Mataifa yote simameni mbele zake Bwana,
    Makabila yote njoni leo nazo ngoma zenu
    Chezeni mbele za Bwana!
    { Wajaluo na waimbe nyimbo
    Wamasai na waruke juu
    Wabaluhyia na wapige ngoma
    Wakikuyu na wacheze sana,
    Watu wote sisimukeni,
    Shangwe nderemo na kelele, pigeni makofi } *2

  2. Vinanda vifijo kelele,
    makofi machezo nderemo
    Kusifu kweli kwawapasa,
    enyi wanyofu wa moyo
  3. Pigieni Mungu kelele,
    imbeni utukufu wake
    Tukuzeni sifa za Mungu,
    tangazeni matendo yake
  4. Shukuruni Bwana kwa zeze,
    kwa kinanda cha nyuzi kumi
    Mfanyieni Bwana shangwe,
    mtumikieni kwa furaha