Mama Akaitika

Mama Akaitika
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumNakaza Mwendo (Vol 19-20)
CategoryBikira Maria
ComposerBernard Mukasa
Views12,037

Mama Akaitika Lyrics

  1. Hatari ikaja nikageuka mbio kumlilia -
    Nikaita mama naye akaitika mwanangu ee
    Akaifungua mikono yake myema kanidaka -
    Nikaita mama naye akaitika mwanangu ee
    Nikalaza kichwa kifuani kwa mama nikihema-
    Nikaita mama naye akaitika mwanangu ee

    |t| Mama anayenipenda, Maria ananijali,
    Popote ninapokwenda, mimi niko salama,
    Nitakimbilia hapo hapo kwa mama wa
    Nitakimbilia hapo hapo kwa mama wa upendo

    |w| Mama yangu Maria nyumba ya salama
    Mama yangu Maria nyumba ya salama
    A hapo hapo kwa mama wa upendo
    Ni hapo hapo kwa mama wa upendo

  2. Wenye nguvu zao walibeba silaha, kupigana -
    Wakapigania ndani ya nyumba yetu, hatari kuu
    Wakazidiana paa wakalipua,tumekwisha -
  3. Kwenye familia migogoro ya ndoa shida tupu -
    Watoto wakawa na maadili duni, balaa tu -
    Na magonjwa lundo uchumi hohehahe, taabu tu
  4. Bibi yangu Eva alizaa laana duniani -
    Mama yangu mwema akazaa wokovu,wa milele
    Nkakabidhiwa niwe mwanaye naye, mamangu ee -
  5. Uovu wa watu ulishika hatamu kila kona -
    Amani ikawa ndoto ya jua kali haipo ee -
    Hofu na mashaka vikafunika nchi,hatari kuu -
  6. Baba wa kanisa akaniita shime tujiunge-
    Tusali rozari tumlilie mama wa amani -
    Atatusikia ataushusha mkono wa Yesu -