Mbegu Nyingine
Mbegu Nyingine Lyrics
- { [s] Mbegu nyingine zikaanguka
[w] Mbegu nyingine (zikaanguka)
Mbegu nyingine zikaanguka penye udongo mzuri! } *2
Zikamea, zikamea na tena zikazaa *2
- Umeijalia nchi na kuistawisha,
Mto wako Bwana umejaa maji mazuri
- Wewe unawaruzuku watu wote nafaka,
Na umeuvika mwaka taji ya wema wako
- Pia na matuta yake maji umeyajaza,
Wapasawazisha popote palipoinuka
- Wailainisha nchi kwa manyunyu ee Bwana,
Hata na mimea yake wewe waibariki
- Kila upitapo kweli pamejaa unono,
Huyadondokeza na malisho yote nyikani
- Na vilima vyote vajifunga nayo furaha,
Na malisho yote yamevikwa nao kondoo