Mbona Nahangaika
| Mbona Nahangaika | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Ikatetemeka Nchi (Vol 3) | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | D. Mdodo | 
| Views | 7,971 | 
Mbona Nahangaika Lyrics
- { Mbona nahangaika, mkiwa mimi,
 Sina hata wa kunifuta machozi } *2
 Ni aibu gani iliyonitanda,
 Najuta hata siku ya kuzaliwa kwangu
 { Maskini mimi, nitakuwa mgeni wa nani,
 Nakulilia e Mungu uniokoe } *2
- Taabu na matatizo yanisonga mimi
 Shida nazo karaha zanisumbua mimi,
 Mungu ufanye hima uniokoe.
- Nimeugua nikilalama, mnyonge mimi,
 Sina rafiki wala mtetezi, mkiwa mimi
 Wote wamenigeuka kuniwinda,
- Kila waliwazalo juu yangu ni baya,
 Kuugua kwangu kumbe ni furaha kwao
 Walitaka nife nisahaulike.
 
  
         
                            