Mimi Mzabibu wa Kweli

Mimi Mzabibu wa Kweli
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumHaya Tazameni (Vol 21)
CategoryMafundisho ya Yesu
ComposerHanga
Views11,192

Mimi Mzabibu wa Kweli Lyrics

  1. [s] Mimi mzabibu wa kweli, mimi mzabibu wa kweli,
    Nanyi m matawi yangu, Baba yangu ni mkulima,
    Mwenye kutunza shamba lake } *2
    [s] Tawi lile lisilozaa
    Baba yangu huliondoa, na kuliteketeza moto,
    [s] Tawi lile linalozaa
    Baba yangu hulisafisha, lidumu katika kuzaa
    Hayo - hayo ni maneno ya Bwana Yesu }*2

  2. Nyinyi mmekwisha, kuwa wasafi,
    Kwa sababu ya neno, nililowaambia
    Kaeni nami, ndani yangu,
    Na mimi na mimi na mimi ndani yenu
  3. Akaaye ndani yangu, huyo atazaa
    Kwani nje yangu, hataweza kuzaa
    Kama vile nje ya mzabibu,
    Tawi halitaweza kamwe kuzaa.
  4. Maneno yangu yakikaa ndani mwenu,
    Ombeni lolote mtatendewa
    Naye Baba yangu atatukuzwa,
    Na nyinyi mtakuwa wanafunzi wangu