Mpendane Daima

Mpendane Daima
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNitachezacheza
CategoryHarusi
ComposerAlfred Ossonga
Views5,385

Mpendane Daima Lyrics

  1. Mungu akaona si vyema mtu huyu awe peke yake
    Nitamfanyia mwenzake yule wanafanana naye
    Akaumba mwanamke, kamleta kwake mwanamume waishi pamoja

    { Ewe Bwana - mpokee mke wako tangu leo
    Ewe Bibi - mpokee mume wako tangu leo
    Muishi nyote pamoja, mpendane daima
    Msitengane daima, msivunje agano } *2

  2. Mungu akawapa uwezo watawale viumbe vyote
    Mungu akasema zaeni muijaze dunia kwa watu
    Baraka za Mungu Baba, zimewashukia tangu leo zaeni matunda
  3. Ewe mwanamume mpende mke wako kwa moyo wote
    Nawe mwanamke heshimu mume wako mtii daima,
    Ndoa ni maagano, kati ya watu wawili wapendanao
  4. Nyumba yenu iwe hekalu lake Mungu kanisa ndogo
    Nyumba ya amani upole na furaha nyumba ya sala
    Mungu ameunganisha mwanadamu asitenganishe daima dawamu