Mshike Mshike
| Mshike Mshike | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mshike Mshike (Vol 5) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 14,529 | 
Mshike Mshike Lyrics
- { Hebu wanadamu na tufikirie sasa ni wapi tutakwenda,
 Vita vimezidi amani hakuna shetani ametia nanga } *2
 Mshike mshike kila kona watu wakimbilia usalama
 Lo! Lo! hili jambo limekuwa kawaida
 Ona wazee na watoto wateseka
 Mshike mshike, mshike mshike
 mshikeshike huu utaisha lini?
 (Tumuombe Mungu), atikise huu mshikemshike
- Ulimwengu wote umekuwa na visa vya ajabu,
 Pande moja vita pande nyingine mambo ya ajabu
 Tujisitiri wapi, kila pande machungu,
 Tunakuomba ee Mwenyezi utupe usalama Baba
- Watu nao wamekuwa wakali kuliko wanyama
 Tunaishi kama hakuna kizazi kingine tena
 Vita vya kila siku, uhasama wa mali,
 Kizazi chetu kimekuwa dhiki tena ukiwa sana
- Ulimwengu nao umekuwa jeneza la vijana,
 Kuvaa vibaya madawa makali wanatumia
 Eti wao wajanja, waenda na wakati
 Hawajui maisha yana mwisho silaha yao pombe
- Hebu fikiria unayefanya mambo haya yote,
 Ujue ya kuwa kila lenye mwanzo linao mwisho,
 Acha ya kidunia, faida ya ukiwa
 Mtegemee Mungu unayo nafasi hii kabla hujafa
 
  
         
                            