Mshipi

Mshipi
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumMSHIPI (VOL. 22)
CategoryZaburi
ComposerE. F. Jissu
Views28,432

Mshipi Lyrics

  1. Ni nani aliye Mungu, Mungu ila Bwana
    Ni nani aliye mwamba, mwamba ila Mungu
    {Ni Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu aha!
    Ni Mungu ndiye kimbilio la unyonge wangu aha!
    Naye anaifanya kamilifu njia yangu } *2

  2. Ni yeye Bwana aliye nguvu zangu nampenda sana
    Ni yeye Jabali langu na boma langu na Mwokozi wangu
    Mungu wangu mwamba wangu ninayemkimbilia
    Ngao yangu na pembe ya wokovu wangu
    na ngome yangu
  3. Katika shida zangu nilimwita Bwana ee Bwana
    Na kumlalamikia Mungu ee Mungu
    Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake
    Kilio changu kikaingia masikioni mwake
  4. Bwana alinitendea sawasawa na haki yangu
    Akanilipa sawasawa na haki yangu
  5. Nitamwita Bwana astahiliye kusifiwa
    Hivyo nitaokoka na adui zangu