Mungu au Shetani
| Mungu au Shetani | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Habari Tuliyoleta (Vol 6) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 10,143 | 
Mungu au Shetani Lyrics
- Ndugu yangu sikia nasema kwa makini,
 Habari hii kuu ya ufalme wa Mungu
 Inasikika sana, sasa imeenea,
 Lakini sio wengi, wanaoiaminiWaimbaji tumeshaimba nyimbo nyingi
 Makasisi wamehubiri pande nyingi
 { Twasema uokoke, nawe wasema kesho
 Inapofika kesho, wasema kesho kutwa
 Siku nazo zapita, miaka inapita
 Uchague mwenyewe, Mungu au shetani } *2
- Ukizipata shida, walaumulaumu,
 Ndugu na majirani, wadhani umelogwa
 Unaanza ugomvi, wachukia wengine,
 Hata bila sababu wawaita wachawi
- Waomba mara moja, ukikosa majibu,
 Kesho inapofika waenda kwa mganga
 Ngoja nikueleze, Mungu hana haraka,
 Jifunze vumilia majibu utapata
- Jifikirie ndugu, usingoje ya kesho,
 Muda ni wako sasa, amua ukubali
 Mengi tumeyasema, ilobaki ni kwako,
 Uchague mwenyewe, Mungu au shetani
 
  
         
                            